[Page principale | Evangile | Cantiques en français | Commentaires et explications sur la Bible | La Bible]

 

Nyimbo Swahili

1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 17, 18, 19, 20, 21, 22, 23, 24, 25,

26, 27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37, 38, 39, 40, 41, 42, 43, 44, 45, 46, 47, 48, 49, 50,

51, 52, 53, 54, 55, 56, 57, 58, 59, 60, 61, 62, 63, 64, 65, 66, 67, 68, 69, 70, 71, 72, 73, 74, 75,

76, 77, 78, 79, 80, 81, 82, 83, 84, 85,

 

1.                       Wimbo 1

Wimbo 1 — kipande 1

 

Tunakuabudu Baba Mungu

Wewe uishie nuruni

Unapambanua mbingu

Twakusanyika mbele yako

Wana wa pendo lako kubwa

Tunasifu jina lako,

{Tunakuheshimu,

Muumba wa vyote

Aleluya ! utukufu,

Kwake Mungu na Mwokozi

Aleluya !}

Wimbo 1 — kipande 2

Wewe ulituangazia,

Mwenye enzi, Baba wa neema,

Kupitia Mwana wako

Kwake tunakubariki,

Twakuabudu, tunakusifu

Na kukutukuza hapa,

{Tunakuheshimu,} etc.

2.                       Wimbo 2

Wimbo 2 — kipande 1

Tuimbe wimbo takatifu

Wakusifu Mwana wa pekee,

Milele Mwana wa Mungu

Kwa kufa na kuishi kwake

Alifunua neema kubwa

Njia  nzuri ya mbinguni

Sifa na heshima

Kwa yesu Mwokozi

Aleluya ! utukufu,

Kwako Bwana !

Aleluya! Aleluya.

Wimbo 2 — kipande 2

Yesu tunakuheshimu

Utakayebaki milele

Wimbo wa wakombolewa.

Uliumizwa tuokoke

Ulichubuliwa tupone

Tuishi kwa ufufuko

Sifa na heshima

Kwa Yesu Mwokozi etc.

3.                       Wimbo 3

Yesu ukombozi wetu

Kwa teso ulitupatia

Ukombozi wa milele

Bwana mwenye utukufu

Ndani yako tuna amani,

Na ushindi na baraka.

Mwokozi muzuri

Uketiye juu

Kwa uzuri

Na heshima

Twakuabudu

Tutakukuza milele.

4.                       Wimbo 4

Wimbo 4 — kipande 1

Tukuzwa Baba wetu (x2)

Uliyetuandalia makao juu mbinguni

Umetowa wokovu (x2)

Wastahili shukrani ya mapendo na kusifu

Wimbo 4 — kipande 2

Tukuzwa Mwana Kondoo (x2)

Kwakuokowa kundi ulikufa msalabani

Ukashinda shetani (x2)

Mukombozi wa ajabu sifa ni kwako milele.

Wimbo 4 — kipande 3

Kweli tukuzwa Bwana (x2)

Pokea pekee nguvu, kuzo, heshima na, ufalme.

Milele na milele (x2)

Tutaimba wokovu, ushindi wa wema wako.

5.                       Wimbo 5

Wimbo 5 — kipande 1

Tukuze Mungu wa mapendo

Wa amani kwa wimbo safi

Aliye kwa wema fahari

funguwa njia  ya mbingu

Kwa neema iliyo bora

Na sisi wabarikiwa,

Hai kwa moyo wa furaha

Tuinuwe nyimbo zetu.

Wimbo 5 — kipande 2

Mioyo yetu yakutukuza

Mwenye uwezo na pendo

Sisi tunakutegemea

Kwa sasa na kwa milele.

Nguvu, wema, neema, uwezo

Ndani yako vinasifu

Na kanisa kwa uhakika

Lakungojea urudi.

6.                       Wimbo 6

Wimbo 6 — kipande 1

Kwa Yesu tunatoa

Zabihu za sifa zetu

Kwa Yesu tunaabudu

Malaika vilevile

Mungu ubarikiwe tunapokusanyika

Wimbo 6 — kipande 2

Tulikuwa zambini

Sote wana wa gazabu

Ukatuweka huru

Ndani yako tuna Baba

Mungu ubarikiwe tunapokusanyika

Wimbo 6 — kipande 3

Na tumepewa Yesu

Na umetuweka kwake

Ndani yake tuliitwa

Kupewa taji milele

Mungu ubarikiwe tunapokusanyika.

Wimbo 6 — kipande 4

Alituahidiya

Mwana aja kututwaa

Kwenye makao ya juu

Tupendapo kumungoja

Mungu ubarikiwe tunapokusanyika.

Wimbo 6 — kipande 5

Hivi tutakukuza

Katika kuzo na nuru

Na tutasema tena

Na Kanisa lako lote

Mungu ubarikiwe tunapokusanyika.

7.                       Wimbo 7

Wimbo 7 — kipande 1

Asifiwe Mwokozi

Na Mwana pekee wa Mungu

Alikuja duniani,

Kuokoa wenye zambi

Ee Yesu utukuzwe milele na milele, (x2).

Wimbo 7 — kipande 2

Ee Mwana ulikuja

Kufa kifo cha aibu

Ukashinda kaburi

Kwa uwezo wa milele

Na Ulivunja nguvu za giza na mauti, (x2).

Wimbo 7 — kipande 3

Kwa pendo ulikunywa

Kikambekichungu sana

Na ukatupatia

Kikombe cha ukombozi

Ee yesu utukuzwe milele na milele, (x2).

8.                       Wimbo 8

Wimbo 8 — kipande 1

Sifa kwa Mwana – Kondoo Mwokozi

Ndani yake kifo kilishindwa

Adui aliona nguvu yake

Vilevile kaburi inamutii

Utukufu kwako Yesu

Utukufu Bwana Yesu

Na kuzimu kumeshindwa

Ushindi (x2).

Wimbo 8 — kipande 2

Vile Kristo alikataliwa

Na kukaa mbinguni aki’ngaa

Na Kanisa lisilo julikana

Karibuni litavikwa utukufu

Utukufu kwako Yesu

Utukufu Bwana Yesu

Na kuzimu kumeshindwa

Ushindi (x2).

Wimbo 8 — kipande 3

Yesu uliahidi kurudi

Kututafuta punde yu waja

Na wafalme katika utukufu

Tutaimba sote wimbo wa ushindi

Utukufu kwako Yesu

Utukufu Bwana Yesu

Na mauti imeshindwa

Ushindi (x2).

9.                       Wimbo 9

Kwa aliye tuokoa

Kwa damu’katusafisha

ufalme na ukuu ni vyake

MwanaKondoo astahili

utajiri, heshima, nguvu,

mamlaka, hekima, na sifa (x2)

10.                  Wimbo 10

Wimbo 10 — kipande 1

Ku’ngaa kwa Sura kamili ya Mungu

Mwana wa milele muabudiwa

Sifa kwako wewe ustahiliye

Kuheshimiwa na wote milele.

Wimbo 10 — kipande 2

Ulishuka ili uwe zabihu,

Kwako tu Mungu akatukuzwa

Utakatifu, upendo, haki yake

Msalaba ukavikuza vyote.

Wimbo 10 — kipande 3

Sasa umeinuliwa kwa Mungu

Karibu na ukubwa mbinguni

Twakuona na utukufu mwingi

Mwana wa watu uliyefufuka.

Wimbo 10 — kipande 4

Twakuabudu wewe ambaye taji

Lakumbusha mateso ya kifo

Bwana Yesu tutakusifu wewe

Tukikizunguka kiti cha enzi

11.                  Wimbo 11

Wimbo 11 — kipande 1

Watoa neema na kuzo

E Bwana Mungu wetu, katika Yesu !

Ubarikiwe na wateule wako

Wenye uheri kukuamini (x2).

Wimbo 11 — kipande 2

Ulitupatia neema,

iliyotupa usalama moyoni :

Wenye heri tutaingia mbinguni

Kunapo’ngaa uso wako (x2).

Wimbo 11 — kipande 3

Wewe watuwekea sifa

Iliyo ya MwanaKondoo mbinguni

Tutakuwa naye katika uheri,

tunda la kazi ya msalaba (x2).

Wimbo 11 — kipande 4

Mungu wa neema na sifa !

Wapendwa wako wanaye Roho wako,

Kwa jina la Yesu tunakuabudu

Yeye ni ukombozi wetu (x2)

12.                  Wimbo 12

Wimbo 12 — kipande 1

kukuimbia Mungu, wa mapendo na kweli

kuabudu, kubariki na kufurahi

kushangilia ushindi wa Bwana Yesu

Ni sehemu tuliyoitwaa kwa imani.

Wimbo 12 — kipande 2

Jina lako lisifiwe, Neema yako

Iliyotujia katika uzuri

Tulikuwa gizani sasa uso wako

Waleta mishale ya nuru mioyoni.

Wimbo 12 — kipande 3

Tupo wana wako, jina nzuri la Baba

Latujaza heri, hakika, amani

Roho wako mhuri, mwangaza na Mwalimu

Na karibu nawe tumekubaliwa.

Wimbo 12 — kipande 4

Ni mapendo yako, kifo, uhai wako

Vilivyotuletea hii sehemu

Kila moja wetu asisahau kamwe

Kwamba tulitakaswa ili tumukuze.

13.                  Wimbo 13

Wimbo 13 — kipande 1

Ukamilifu usiyoweza kusemwa

Wa uwezo, mapendo, hakiba’siyokwisha, – isiyokwisha

Mwana wa Mungu milele !

Utukufu wa mbinguni

Kwa amani yako, Kanisa lako pe ndwa

Lainama kuabudu (ter)

Wimbo 13 — kipande 2

Wakaa ee Yesu, kwa kuume kwa Baba

Ukivikwa uwezo, nuru, utukufu – na utukufu

Mungu wetu (x2)

Mioyo zetu (x2)

Yainama mbele yako kwa kutii

Pia kukuinua (ter).

14.                  Wimbo 14

Wimbo 14 — kipande 1

Mbinguni kwa kiti cha Baba

Twakuona ee Mwokozi

Pumzikoni vile nuruni

Una uwezo na ku’ngaa

Kazi ya neema imekwisha:

Umekaa patakatifu ;

Juu utukufu umepewa

Watawala juu ya vyote.

Wimbo 14 — kipande 2

Twashinda kwa ushindi wako

Yesu Mwokozi muweza,

Juu katika utukufu

Umetangulia wako !

Tuna tumaini la mbingu,

Linalokutegemea

Tuna uhakika wa roho

Ni Musingi wa imani.

Wimbo 14 — kipande 3

Sifa kwa kichwa cha kanisa!

Bibi arusi mupendwa

Pande zako punde atakaa,

Akibariki milele

Wewe Bwana mwenye uzuri

Tutakaofurahia,

Na pendo lako la ajabu

Litakuwa siku zote.

15.                  Wimbo 15

Wimbo 15 — kipande 1

Mungu wa pendo na neema!

Twafurahi kukutana

Mbele ya uso wako mzuri

Kuabudu na kubariki

Na Katika salama yako

Kweli Upewe ibada,

Iletayo mashukurani,

Marashi : jina la Yesu.

Wimbo 15 — kipande 2

Bwana ingia nafsi zetu

Na wema wako wa ajabu,

Utuwashie moto wako

Wa pendo lako Ee Bwana ;

Ndipo sifa zitatokea

Mioyoni mwetu kwa Roho

Ili tuimbe rehema zako

Na pendo ndani ya Yesu.

Wimbo 15 — kipande 3

Tunapenda kuketi pale

Twawekwa na kazi  yake

Na tunafuata nyayo zake,

Hadi mbinguni alipo

Ni pahali patakatifu

Ambapo mlango ni wazi

Sifa za waamini zapanda

Kwako  kupitia Yesu

16.                  Wimbo 16

Wimbo 16 — kipande 1

Umoja wa Kanisa wapendeza

Bwana Yesu, wakufurahisha

Kwa kulipenda ulijitolea

Wataka liwe nawe mbinguni

Wimbo 16 — kipande 2

Roho yako Yesu yatukusanya

Karibu nawe katika pendo

Heri gani kukuabudu pamoja

Twatangaza kufa na kurudi

Wimbo 16 — kipande 3

Ni kutamu ndugu wakikuabudu

Roho wako akiwa kiongozi

Katika nyimbo na maombi yetu

Tunayokutolea pamoja.

Wimbo 16 — kipande 4

Ni kweli palipo uwepo wako

ukileta uhuru moyoni

kila mwamini katika amani

asikia nguvu, uhakika.

Wimbo 16 — kipande 5

Na Itakuwaje kwa mukutano

Mbinguni kanisa litakuona

Furaha gani isiyo na mwisho

utukufuni likikuabudu.

17.                  Wimbo 17

Wimbo 17 — kipande 1

Ulitualika, tena kwa siku hii

Mwokozi Muabudiwa ili tulishwe

Katikati ya jangwa, wajenga meza hii

Kumbusho la pendo lako (x2).

Wimbo 17 — kipande 2

Kando yako, Bwana,kanisa lazunguka

Kukumbusha kifo chako hadi urudi,

Twavunja mukate, tunakunywa kikombe,

Kumbusho la pendo lako (x2)

Wimbo 17 — kipande 3

Uovu wetu ulikulemea kichwani

Mzigo wa uchungu na muzito sana;

Lakini kwa amani, tunasherekea

Kumbusho la pendo lako (x2)

Wimbo 17 — kipande 4

Tukionja mkate huu, na kinywaji hiki

Vinaelekeza macho yetu juu.

Na Punde tutamaliza safari yetu

Tutatambua u pendo (x2)

Wimbo 17 — kipande 5

Asante Yesu, Mwokozi na Mwaminifu!

Bila kivli tutakuona mbinguni

Na tutatukuza, kwa sifa ya milele,

Ukubwa wa pendo lako (x2)

18.                  Wimbo 18

Wimbo 18 — kipande 1

Mbele ya kiti cha baba

Akaapo kwa heshima

Jicho letu latazama

Uzuri wako Bwana

Utukufu ulio nao

Ndani ya ku’ngaa kwako

Watuangazia kweli ndani ya mioyo yetu

Wimbo 18 — kipande 2

Kungaa kwa uso wako

Siko  kuvutiapo tu

Kwani neema yako kubwa

Yaangaa usoni mwako

Kwa neema ulishuka

Duniani mwa uasi

Ulipotuchukulia maovu  hata  zambi

Wimbo 18 — kipande 3

Nafsi yashangaa sana

Juu ya upendo huu

Ulio mukubwa sana

Hauna hata mpaka

Hivyo sisi twatamani

Kurudi kwako hapa

Ili tuone, tutamke

Makuu ya pendo lako.

19.                  Wimbo 19

Wimbo 19 — kipande 1

Tukaribie na kwa nyimbo zetu

Mwana Kondoo mupendwa akuzwe

Alishinda na alifufuka

Tutangaze makuu yake yote

Sisi wenye : kupendwa na Kristo (x2)

Wimbo 19 — kipande 2

Alitufilia kama sadaka

Tukapokea upendo wake

Kwa kutuokoa katika giza

Alikubali fimbo za uhaki

Akafanywa : chukizo, laana (x2)

Wimbo 19 — kipande 3

Twakuabudu sadaka ya toleo

Wewe ulitununua sisi

Tukumbushapo kifo, mateso

Tunangoja siku yakuonekana

Mbinguni : kama bibi arusi (x2).

Wimbo 19 — kipande 4

Tunasherekea kwa meza hii

Pendo la Kondoo uliyechinjwa

Kwako roho zetu zinalindwa

Zikionja salama na uheri

Na kwa bei ulivinunua : ulivinunua (x2).

20.                  Wimbo 20

Wimbo 20 — kipande 1

Mbele ya kiti cha neema

Twakuabudu Mungu wetu

Tukiingia patakatifu

Kwa njia ya Yesu Kristo.

Wimbo 20 — kipande 2

Mkate wa juu ushibishao

Ni chakula chetu kweli

Ndani ya Yesu tumepewa

Uzima unaodumu.

Wimbo 20 — kipande 3

Pa’li pa kikombe  kikali

Ulichomunywesha, Mungu

Mwokozi mwema na mupole

Ametupa cha wokovu.

Wimbo 20 — kipande 4

Kwa sauti ya malaika

Tukinyakuliwa juu

Tutamuimbia sifa zake

Tutamuona…  siku nzuri !

21.                  Wimbo 21

Wimbo 21 — kipande 1

Yesu sadaka ya Mungu

Ulishuka duniani

Ukafunga ile shimo

Itutengayo naye.

Wimbo 21 — kipande 2

Ukavaa mwili wa mutu

Ukateswa kabisa ;

Kwa Kuokoa kiumbe

Ukapata uchungu.

Wimbo 21 — kipande 3

Ni wewe hekima yetu

Uhai na salama

Kimbilio kwa mateso

Wokovu wa milele.

Wimbo 21 — kipande 4

Ee Mwokozi mwaminifu

Twabaki ndani yako

Hadi uzima milele

Waishi tutaishi.

22.                  Wimbo 22

Wimbo 22 — kipande 1

Kwa kutuokoa, Bwana wa uzima

Alisumbuliwa na kuaibiwa

Sifa kwake  Mwana

Sifa kwako Kondoo

Pokea mioyo yetu, mshahara wako

Ulioupewa, kwa mlima kalvari.

Wimbo 22 — kipande 2

Kifo chako Yesu, kikaosha zambi

Ukafunga shimo kwa miguu yetu

Sifa kwake Mwana

Sifa kwako Kondoo

Twakusifu Bwana, ulitupa amani

Heri, ukombozi kwa mateso yako.

Wimbo 22 — kipande 3

Kututajirisha, mwenyewe mbinguni

Ukawa  maskini, wewe Mungu  mkubwa

Sfa kwake Mwana

Sifa kwako Kondoo

Pokea mapendo na heshima zetu

Viwe kwako Mungu pasipo mwengine.

Wimbo 22 — kipande 4

Mema ya pendo lako Mchungaji wetu

Unatuandalia meza kila siku

Sifa kwake Mwana

Sifa kwako Kondoo

Wapendwa wako Bwana wanafurahi

Wakionja pendo na matunzo yako.

Wimbo 22 — kipande 5

Kwa amani twafwata uriti wetu

Wewe ni sehemu yetu kwa milele

Sifa kwake Mwana

Sifa kwako Kondoo

Mukombozi Mungu, unayetupenda

Upewe nguvu, ufalme na heshima.

Wimbo 22 — kipande 6

Milele na milele tutakusifu

Pendo lako kubwa na ushindi wako

Sifa kwake Mwana

Sifa kwako Kondoo

Pokea mioyo yetu, mshahara wako

Ulioupewa, kwa mlima kalvari.

23.                  Wimbo 23

Wimbo 23 — kipande 1

Nani atatukuza, nani atatambua,

Pendo lililokushusha toka mbinguni

Kwenda Getsemane,...Golgota ya damu

Pale ulipochomwa mkuki na Mungu.

Wimbo 23 — kipande 2

Siyo wale, Bwana, majeshi wa mbinguni,

Ama vile vyote ambavyo uliumba

Ama urefu wa bahari na mbingu,

Vitakavyotukuza upendo wako.

Wimbo 23 — kipande 3

Yesu ! Pendo lako na neema yako nzuri,

Nani atavikuza ? ni sisi waovu tu

Uliofanya wafalme, makuhani,

Kwa ajili yao ulionja kifo.

Wimbo 23 — kipande 4

Wakombolewa tu, kwa raha takatifu,

Wataimba wema wako na kubariki.

Uliwanunua, Ee Yesu, kwa damu

Watakuwa nawe milele mbinguni.

24.                  Wimbo 24

Wimbo 24 — kipande 1

Twakuona ukiangaika

Ukinywa kikombe kile

Tunakuona ukijitoa

Mtakatifu kwetu waovu.

Wimbo 24 — kipande 2

Kifo chako sadaka safi

Tukitazame daima

Damu yako ilituosha,

Ikatufungulia mbingu.

Wimbo 24 — kipande 3

Pendo lako ni kubwa Kristo

Linagusa mioyo  zetu

Ulifilia ulimwengu

Wewe ndiye Mwokozi wetu.

25.                  Wimbo 25

Wimbo 25 — kipande 1

Kama Kondoo ulikufa, Yesu

Kwa zambi zetu, Mukombozi wetu

Pendo gani ? ni pendo la ajabu

Kwa kutuokoa, Yesu ukafa.

Wimbo 25 — kipande 2

Kwa ule wakati zambi zetu

Zilikuletea azabu kali

Kwa kufa ukavunja minyororo

Ukatuletea neema, raha.

Wimbo 25 — kipande 3

Amen ! Bwana ! Uwezo na sifa

Kwako heshima, hekima, ufalme

Tangu sasa tunasema na wewe :

Ubarikiwe Ee Mukombozi.

26.                  Wimbo 26

MwanaKondoo uliteswa

Ukachukua taabu yetu

Na ukatufanya kwa Baba

Wafalme na makuhani

Pamoja tunakuheshimu

Twakusifu na kukuinua

Nguvu, ufalme pia kutii

Mioyoni tunakuabudu

Amen ! Amen ! Bwana ! Amen.

27.                  Wimbo 27

Wimbo 27 — kipande 1

Twakuona utukufuni

Ee Mwokozi !

Tukionja ushindi wako

Mwenye nguvu

Milele pamoja na Mungu

Kwa kuume kwa Baba Mungu

Uliyeshuka duniani

Na upole.

Wimbo 27 — kipande 2

Kwa sisi ukawa laana

Ee Mwokozi !

Ukateswa zaidi sana

Ee Mwokozi !

Damu ’katoka mbavu zako

Ukatuondolea zambi

Kwa kufa kwako tunaishi

Ee Mwokozi.

Wimbo 27 — kipande 3

Tunakungoja toka mbingu

Ee Mwokozi !

Ulisema waja kututwaa

Yesu mweza !

Furaha isiyo na mwisho

Yakutazama sura yako

Na vile yakukufanana

Ee Mwokozi.

28.                  Wimbo 28

Yesu, neema, damu yako

Na musalaba wako

Kungaa kwa uso wako

Vyatupatia haki

Nafsi yetu yapumzika

Ndani yako Mwokozi

Wewe mwanzo na chemchemu

Ya uheri milele.

29.                  Wimbo 29

Wimbo 29 — kipande 1

Katupenda mpaka kufa

Mwokozi wa mapendo

‘Katushindia shetani

Hadi kwa ngome yake, (x2).

Wimbo 29 — kipande 2

Namna vilikulemea

Pekee kwa saa ya giza

Kuachwa pia na hofu

Ya zambi zetu nyingi, (x2).

Wimbo 29 — kipande 3

Sasa fujo ya mawimbi

Yaliyokufikia

‘katuletea pumziko

Ya kazi yako nzuri, (x2).

Wimbo 29 — kipande 4

Kando yako wateule

Wako hapa duniani

Sasa wanaonja raha

Ya nyumba yake Baba, (x2).

30.                  Wimbo 30

Wimbo 30 — kipande 1

Kondoo wa Mungu Kristo akafa

Mutini (x2)

Pazia pale ’kapasuka

Kwa muti (x2)

Kwa patakatifu sana,

Mbele ya Mungu twafika

Kwako Yesu uliyejitoa

Mutini (x2)

Wimbo 30 — kipande 2

Uliinuliwa toka chini

Mutini (x2)

Ulikunywa kikombe chetu

Mutini (x2)

Kwa pendo ‘kakimaliza

Damu yako ilituosha

Tumeokoka kwa milele

Kwa muti (x2)

Wimbo 30 — kipande 3

Hayani sifa zako ‘kangaa

Mutini (x2)

Yesu uliupata ushindi

Mutini (x2)

Milele upewe  nguvu,

Heshima na sifa nyingi

Kwa sababu ulishinda

Mutini (x2)

31.                  Wimbo 31

Wimbo 31 — kipande 1

Nyimbo za mbinguni

Ni nzuri sana

Vinanda na nyimbo

Jaeni mbingu

Kwa nafasi kubwa,

ule wimbo mpya

Daima waanza

Kando ya Kondoo.

Wimbo 31 — kipande 2

Kwa kiti cha enzi

Tutakuona

Ukivikwa taji

Za kila aina

Na mikono yako

Inaonyesha

Ginsi uliteswa

Kwa musalaba

Wimbo 31 — kipande 3

Neema ya milele!

Uliye chinjwa

Ukajitolea,

‘Kamwanga damu

Kwa patakatifu,

Uheshimiwe

Mungu Baba yako

Aabudiwe.

Wimbo 31 — kipande 4

Nyimbo za mbinguni

Ni nzuri sana

Vinanda na nyimbo,

Vyajaa mbingu

Heshima na nguvu,

Kuzo milele

Kwa Mungu mushindi,

Na Kondoo wake.

32.                  Wimbo 32

Wimbo 32 — kipande 1

Mwana wa Mungu, wa ajabu

Waonekana  usoni

Upendo muzuri wa Baba

Hata sifa zake nyingi

Washika dunia mkononi

Uliitosha utupuni

Vyote vinaimba Hekima,

Na kuzo lako Muweza.

Wimbo 32 — kipande 2

Mbele ya Baba kifuani

Wamupendeza daima

Mupo mumoja uwezoni

Mupo mumoja pendoni

Ulipenda, siri ya ajabu

Kutoka patakatifu

Kuja dunia yenye zambi

Ili ufe Mwana Kondoo.

Wimbo 32 — kipande 3

Upendo, neema ya ajabu

Twakuona Mutu, Mungu

Kwa sanduku hadi kalvari

Ukifwata njia chungu

Mugeni, ulikataliwa

Hata na walio wako

Ukanywa kikombe kichungu

Shambani mwa Getsemane.

Wimbo 32 — kipande 4

Ukabeba, Mwana Kondoo

Kwa saa za giza mutini

Hukumu ya makosa yetu

Pia gazabu ya Mungu

Ee Bwana tutakutukuza

Milele kule mbinguni,

Na roho zetu zitaimba

Pendo lishindalo kifo.

33.                  Wimbo 33

Wimbo 33 — kipande 1

Yesu rafiki yetu mkubwa

Pendo gani !

Atupenda kushinda ndugu

Pendo gani !

Jamaa, rafiki, wanapita

Heri yaja na kutoweka

Moyo wake tu hauchoke

Pendo gani

Wimbo 33 — kipande 2

Yu uzima wetu milele

Pendo gani!

Na kwa milele tutukuze

Kazi yake !

Kwa damu yake tumeoshwa

Alipotukuta jangwani

Kwa neema akatuokoa

Pendo gani !

Wimbo 33 — kipande 3

Alijitoa kama zabihu

Pendo gani!

Anapenda kutubariki

Pendo gani!

Nafsi yetu imusikie

Kwa amani, kamwe, isiogope

Iishi karibu na Yeye

Kwa upendo.

34.                  Wimbo 34

Wimbo 34 — kipande 1

Kazi ya milele, tutakapo pumzika

Bila mwishowako watakuabudu

Wakitupa taji juu ya miguu yako

Wakistaajabu na watainama, (x2).

Wimbo 34 — kipande 2

Tutautazama uso wa Muabudiwa,

Uzuri wa Mwokozi, Bwana Arusi

Na tutavumbua fumbo isiyopimwa

Ya neema na mapendo bila mpaka, (x2).

Wimbo 34 — kipande 3

Kwako pekee Yesu, kwa nuru yako nzuri

Wewe jua la haki liangazalo

Kanisa litavaakatika utukufu

Nuru safi ya ukamlifu wako, (x2).

Wimbo 34 — kipande 4

Utaona pekee lile unalotaka !

Tunda kamili la kazi ya msalaba

Utafurahia kazi ya nafsi yako

Mapendo yako Mungu yatatosheka, (x2).

35.                  Wimbo 35

Wimbo 35 — kipande 1

Twaishi kwako, chemchemu njema

Tufurahie nuru yako

Kukuona mbele ya Baba

Yesu, pumziko ya roho yetu.

Wimbo 35 — kipande 2

Mungu alitutolea Yesu

Na kwake akaleta amani

Akapendezwa na uhaki

Deni yetu kweli imelipwa.

Wimbo 35 — kipande 3

Tuna heri, Bwana wema wako

Umetufungulia mbingu

Na mukristo kwa utulivu

Aingia kwani ameokoka.

Wimbo 35 — kipande 4

Kwa nini tusikupende Yesu ?

Uliyejitolea kwetu

Wewe ambaye pendo lako

Laja kila siku mbele yetu.

36.                  Wimbo 36

Wimbo 36 — kipande 1

Watufunza, watufariji

Yesu ukiwa mbinguni

Kwani Roho na neno Lako

Vyabaki na wateule.

Wimbo 36 — kipande 2

Twasikia sauti yako

Kupitia neno Lako

Roho wako hufahamisha

Agusa moyo na macho.

Wimbo 36 — kipande 3

Kumbukumbu La pendo Lako

Lafikiawalio wako

Katika Jangwa watukuzwa

Twaonja mema ya mbingu.

Wimbo 36 — kipande 4

Hilini Neno La uzima,

Kama tunda La Eskoli

Linalotupatia nguvu

Jangwani tulikulapo.

Wimbo 36 — kipande 5

Muda kitambo kazi yake

Itakwisha kwa kundi hii

Tutakapo kuona nuruni

Tutazungumuza nawe.

37.                  Wimbo 37

Wimbo 37 — kipande 1

Yesu, Nguvu, Mwamba wangu

Mwokozi wangu mkuu

Adui hawataweza

Nikilindwa nawe.

Wimbo 37 — kipande 2

Kwa Neema ulinisamehe

Umenipa mbingu

Ninazungukwa na nguvu

Imani yatosha.

Wimbo 37 — kipande 3

Wewe ndiye Mukombozi

Na mwenye upendo

Wewe ni uheri, sifa

Na Mwokozi wangu.

38.                  Wimbo 38

Wimbo 38 — kipande 1

Neno lako ni aminifu

Bwana halipite kamwe

Nafsi yangu iliaminiyo

Haitaogopa tena.

Wimbo 38 — kipande 2

Ninajuwaee wazo nzuri

Miongoni mwa kondoo zako

Hakutapotea yoyote

Mchungaji uliahidi.

Wimbo 38 — kipande 3

Wana wa pendo lako kubwa

Tupokifuani mwako

Hata dunia na kuzimu

Havitatutosha kwako.

39.                  Wimbo 39

Wimbo 39 — kipande 1

Bwana wangu mwema

Uliniponya

Nipo mushahara

Kwa kazi yako

Nilikuwa mnyonge

Sasa ni wako

Neema yako nzuri

Kaniokowa.

Wimbo 39 — kipande 2

Chunga kwa rehema

Nafsi milele

Katika furaha

Na usalama

Unishike mkono,

Nisilegeye

Nichunge daima

Karibu nawe.

40.                  Wimbo 40

Wimbo 40 — kipande 1

Ni ndani ya Mungu

Kwa tumaini lote

Mioyo yapumzika

Uvumilivu wako,

Rehema yako kubwa

Vinanionyesha

Matunzo ya pendo.

Wimbo 40 — kipande 2

Ni kutamu kwangu !

Kuwa wewe ni Baba

Yu nami popote

Waniangazia neema

Wapokea maombi

Unanitazama,

Wanipa imani.

Wimbo 40 — kipande 3

Salama na pendo

Furaha kamilifu

Ni vyangu milele

Naona mbele yangu

Njia nzuri ya raha

Ni ya utukufu

Yaenda mbinguni.

Wimbo 40 — kipande 4

Bwana niongoze

Ukinishika mkono

Linda nyayo zangu

Mungu kwa pendo lako

Nguvu, hekima yako

Vinatuzunguka

Ni msaada wa nguvu.

41.                  Wimbo 41

Wimbo 41 — kipande 1

Nikufikilipo Bwana

Pia neema yako

Moyo wangu wafurahi

Kwani utakuona, (x2).

Wimbo 41 — kipande 2

Hata kama ninachoka

Ninasonga mbele tu

Kama mahali pakavu

Kunakoota miiba, (x2).

Wimbo 41 — kipande 3

Hata adui ni wengi

Kwa kunishambulia

Kwa mitego ya hatari

Wanizunguka sana, (x2).

Wimbo 41 — kipande 4

Ninaweza kila siku

Kufuata njia yako

Na kwa pendo lako kubwa

Kuonja lifaalo, (x2).

Wimbo 41 — kipande 5

Bwana, pumziko na Mwamba

Wokovu, haki yangu

Wanikaribia mimi

Wanipendeza mimi, (x2).

Wimbo 41 — kipande 6

Yesu, Mukombozi wangu

Nijaze uhodari

Wezesha mtumishi wako

Akuwe mwaminifu, (x2).

Wimbo 41 — kipande 7

Hadi siku wateule

Washindi ndani yako

Wakivaa kanzu nyeupe

Watakuona kuzoni, (x2).

42.                  Wimbo 42

Tumutazamie Yesu,

Bado kitambo Mwokozi

Atarudi toka mbingu,

Katika kungoja kwa heri

Nafsi zetu ziwe tayari

Tuwe macho, tusilale

Wakristo, Mwokozi aja.

43.                  Wimbo 43

Wimbo 43 — kipande 1

Kamwe sitapungukiwa

Kwani Bwana ni Mchungaji

Ninaishi chini ya gongo

La asiyebadilika

Kweli Yesu ulinitia

Miongoni mwa kondoo zako.

Wimbo 43 — kipande 2

Ulinipa salama yako

Najua ulinipenda

Nikipita katika moto

Najua sitaungua

Macho yako ni juu yangu

Ongoza yangu juu yako.

Wimbo 43 — kipande 3

Bwana nikukaribiapo

Sioni woga yeyote

Neema yako ni mwamba mkubwa

Kimbilio haki kwangu

Ulinishika mkononi

Shetani hata nitosha.

44.                  Wimbo 44

Tufurahi wakristo, (x2) ;

Bado kitambo Yesu,

Ndani mwetu atatukuzwa

Bwana utarudia, (x2)

Tutakutana nawe

Na tutaishi ushindi.

45.                  Wimbo 45

Wimbo 45 — kipande 1

Siku gani tutaona

Kanana ya mbinguni ?

Juu ya mbingu mwasikia ?

kristo anatuita.

Na tutaishi naye,

zoruba itakoma

Tutaimba kwa milele

wimbo wa salama.

{Heri kamilifu, Uheri, uheri

Heri kamilifu, Pumziko ni Bwana

Kanisa litakapokusanyika mbinguni

Litaimba bila mwisho :

Sifa kwake Kondoo.}

Wimbo 45 — kipande 2

Wateule wataona,

utukufu wa Kristo

Wakiwa wamefufuka,

watamshuhudia

Wakisifu ushindi,

kazi ya musalaba

Pamoja kando ya kiti,

tutampa naziri.

Wimbo 45 — kipande 3

Kama kule juu mbinguni,

mwenye zambi akitubu,

Malaika kwa umoja,

wabariki Bwana

Itakuwa furaha,

wakati kundi lake

Litakapo kombolewa,

nakushinda vyote.

Wimbo 45 — kipande 4

Kanana ni fasi nzuri,

Ni inchi ya ahadi

Tukikusanywa na Mungu,

kwa upendo wake

Tutaimba milele

wimbo wa kufurahi

Utasikika mbinguni,

Milele daima.

Wimbo 45 — kipande 5

Siku hiyo ya milele,

itaangaa asubui

Sote katika umoja

Na mapendo pia

Na tutasema tena

Na yule Muabudiwa :

Mwana Kondoo astahili

nguvu na mamlaka

{Heri kamilifu, uheri, uheri} etc.

46.                  Wimbo 46

Wimbo 46 — kipande 1

Niwapo na fasi mbinguni

Hapa chini nina amani ya roho

Mbali ya mawimbi na zoruba

Niwezapo pumzisha kichwa

Kifuani mwa Mwokozi

Wimbo 46 — kipande 2

Juu nyumbani mwa Baba yangu

Ndani yako Yesu nina vyote

Vyote vya pa’li patakatifu

Bwana, uso wako, nuru yangu

Wanipa sifa na pendo.

47.                  Wimbo 47

Wimbo 47 — kipande 1

Tunaweza kukufuata

Njiani mwako Yesu

Ulimopenda kuishi

Ukiwa mgeni kwetu

Ulikuwa pekee yako

Ukitenda mema tu

Katika njia hii nzuri

Yako mtu mkamilifu.

Wimbo 47 — kipande 2

Hiyo njia yafungua

Mema, mali ya pendo

Mungu mwenyewe atambua

Humo utakatifu

Hivi kwa neema yako

Twaweza kukufuata

Kwani ulituokoa.

Wabarikiwa wako.

Wimbo 47 — kipande 3

Mwili wetu ukiteswa

Sikitiko na taabu

Tunapoonja uchungu

Tukufuatapo, Yesu

Juu yako twatazamia

Katika uzaifu

Ili utuonyeshe

Utakatifu wako.

Wimbo 47 — kipande 4

Njia hii yaishia

Inchini penye sifa

Palipo uso wa Mungu

Na wa Mutu mushindi

Tukiwa wakamilifu

Kuzoni tutaabudu

Yesu tutakufanana

Tutashibishwa nawe.

48.                  Wimbo 48

Wimbo 48 — kipande 1

Jangwani nifuatamo njia yangu

Kuelekea inchi ya kuishi,

Kusiwe kizuizo hata kazi

Kwani mbingu ni uriti wangu.

Wimbo 48 — kipande 2

Mwokozi ni Kiongozi, tumaini

Nichunge na hatari ya siku.

Uniangazie kwa usiku

Unichunge pendoni mwako.

Wimbo 48 — kipande 3

Kila asubui mapendo yako

Yanitumia kila siku mukate.

Jioni ninapolala salama

Wewe unahusika na kesho.

Wimbo 48 — kipande 4

Mwamba wangu ! Maji safi ya neema

Yatiririka kuniondolea kiu

Kwa Roho wako unichunge

Moyo wangu usinungunike.

Wimbo 48 — kipande 5

Hivi sasa mwisho wa njia yangu

Utaniletea pumuziko ;

ushuhuda hakika wa Bwana

Unanikinga na mawimbi.

Wimbo 48 — kipande 6

Inchi yangu, ee inchi ya ahadi

Moyo wangu sasa wakusalimu

Katika raha tele takatifu

Jina lako Mungu lisifiwe.

49.                  Wimbo 49

Wimbo 49 — kipande 1

Kuokolewa kutoka inchi

Ya utumwa, zambi, giza

Tunatarajia uriti

Tukiongozwa na Roho.

Wimbo 49 — kipande 2

Huko hatutalia tena

Kazi, kiu vile njaa

Hakuna hatari, kilio

Ni amani, uheri tu.

Wimbo 49 — kipande 3

Milele pamoja na Kundi

Upendoni kwa furaha

Tutakusifu kwa milele

Kondoo uliyetufia.

50.                  Wimbo 50

Wimbo 50 — kipande 1

Kujeni wapendwa, tuchote kwa furaha

Amani na neema kwa chemchemu

Tutangaze mema, tuinue upendo

Wa Mwokozi anayetuponya, (x2).

Wimbo 50 — kipande 2

Tutakutukuza, Bwana nyimboni mwetu

Tunaojua mapendo yako

Ulitutendea mambo mazuri sana

Tutakubariki siku zote, (x2).

Wimbo 50 — kipande 3

Twakuabudu Yesu, Mwokozi wa mapendo

Uliyetuokoa kwa damu

Twaimba upendo wako hapa duniani

Mbinguni tutauimba daima, (x2).

51.                  Wimbo 51

Wimbo 51 — kipande 1

Furaha gani, tunyakuliwapo

Yesu akirudi

Na milele Kanisa litakwenda

Mbali ya dunia, (x2).

Wimbo 51 — kipande 2

Wakati mzuri, Kristo atatuleta

Karibu ya Baba

Tutakapotukuzwa mbele yake

Kristo atatuingiza, (x2).

Wimbo 51 — kipande 3

Kutasikika kule juu mbinguni

Nyimbo za heri tu

Wote watatangaza neema yake

Pendo la Mwokozi, (x2).

Wimbo 51 — kipande 4

Shuka mbinguni, tunakuhitaji

Twakupenda, kuja

Tangu zamani tunakungojea

Bwana arusi njoo, (x2).

52.                  Wimbo 52

Wimbo 52 — kipande 1

Wateulewako

Katikavita,

Wakutapohapa

Unyongemwingi,

Mbinguniwabebwa

Moyonimwako

Eekuhaniwetu

Mukubwasana.

Wimbo 52 — kipande 2

Ukijaanawema

Napendopia

Hautamsahau

Mukombolewa

Niwewemsaada

Katikavita

Unatutetea

Mungu Mtetezi.

Wimbo 52 — kipande 3

Kwakilauchafu

Niwewepekee

Utusafishaye

Miguukwamaji

Wasema : mwamini

« Niigemimi

Mufanokamili

Mtumishimwema. »

Wimbo 52 — kipande 4

Tundalaushindi,

Wakombolewa,

Watakuwanawe

Kuzonimwako

Nyumbanimwa Baba

Usonimwake

Tumepewakazi :

Nipendolako.

53.                  Wimbo 53

Wimbo 53 — kipande 1

Neema gani Bwana, kuitwa ndugu zako

Na kuwa na amani, tukikungojea

Ulitufungua kutoka shida zetu

Haki yetu, pendo lako, (x2).

Wimbo 53 — kipande 2

Ni wewe uliyetusafisha kwa damu

Na moiyoni mwetu, ukaleta amani,

Yesu, mkate wa juu, chakula cha mbinguni,

Kwako tupo wa milele, (x2).

54.                  Wimbo 54

Wimbo 54 — kipande 1

Mshindi wa shetani na dunia

Bwana Yesu amefufuka

Na Kwa woga wa giza kubwa

Siku nzuri inafwata

Hakuna woga, ziki tena

Enyi taifa teule,

Pamoja na furaha tele

Tuimbe Yesu amefufuka.

Wimbo 54 — kipande 2

Siku yaja ya raha kubwa

Mwili huu utainuka

Umepandwa muharibifu

Utafufuka kuzoni

Miili yetu ya uzaifu

Itakapobadilishwa

Yesu utaifananisha

Na mwili wako wa kuzo .

Wimbo 54 — kipande 3

Tayari kwa uhai wako

Yesu tumefufuliwa

Ndani yako, kwa neema yako

Tumepanda juu mbinguni

Kwa kungojea siku yako

Itakayoonekana

Tukikutegemea wewe

Tunapiga vita nzuri.

55.                  Wimbo 55

Wimbo 55 — kipande 1

Ni kutamu kupenda Mungu Baba

Kumwendea sawa, bila woga

Kufanya kazi hapa duniani

Tukiongozwa na Roho wa Bwana.

Wimbo 55 — kipande 2

Ni kutamu kupata kwa saa zote

Rafiki mpendwa na msaidizi

Kuwa huru kuingia mbele yako

Kupata msaada hatarini !

Wimbo 55 — kipande 3

Ni kutamu kuwaza neema yako,

Kwa Uzaifu na ulegevu

Na kusema : Alitwaa fasi yetu

Akateswa kama Mwana Kondoo

Wimbo 55 — kipande 3

Ni kutamu kuona sifa zako,

Bwana Yesu, na watakatifu,

Kungoja kwa salama siku yako

Ya ushindi bei ya imani !

Wimbo 55 — kipande 4

Siku gani mbele ya kiti chako,

Watakatifu wametukuzwa,

Kila moja akivaa taji yake

Wataziweka kwa miguu yako !

56.                  Wimbo 56

Wimbo 56 — kipande 1

Haki yako kamili, safi,

Ee Mwokozi ni uzuri

Na kuonekana kwa heshima

Kwa aliye kombolewa.

Wimbo 56 — kipande 2

Uliturehemu kabisa

Na tumepewa zawadi

Pia uhakika imara

Twangojea siku kubwa.

Wimbo 56 — kipande 3

Kwetu taifa kamilifu,

Hakuna tena hukumu

Hakuna pia woga kwetu !

Mungu alitusamehe.

Wimbo 56 — kipande 4

Yesu wewe ni haki yetu,

Wasema : “naja upesi”

Kanisa lote lifurahi,

Kukuona Mukombozi !

57.                  Wimbo 57

Wimbo 57 — kipande 1

Ndugu sote tusimame

Tuna Mwalimu hapa

Bwana arusi yu aja

Kristo ataonekana, (x2).

Wimbo 57 — kipande 2

Karibu atatawala

Pamoja na kanisa

Punde atalivika taji

La sifa ya ahadi, (x2).

Wimbo 57 — kipande 3

Usiogope kundi ndogo

Wewe mpendwa wa Baba

Msalaba wa Mwana Kondoo

Uwe bendera yako, (x2).

Wimbo 57 — kipande 4

Dunia ikikuchukia

Chuki yake ni kuzo,

Pendo, tumaini, imani

Vitakupa ushindi, (x2).

Wimbo 57 — kipande 5

Sifa kwa Yesu Mwokozi

Tunamutumainia

Heri anayemuabudu

Ndani ya moyo wake, (x2).

58.                  Wimbo 58

Wimbo 58 — kipande 1

Tunainua, ee Baba mpenzi

Kwako mioyo yetu na mikono

Na maombi twakutolea

Pendoni safi na ukweli

Kama waabudu wa kweli.

Wimbo 58 — kipande 2

Mbele yako twajisikia

Kama tumepewa Mwana wako

Wana wa neema yako ya mbingu

Tuna fasi rohoni mwako

Kama Yesu na rafiki.

Wimbo 58 — kipande 3

Tumependwa jinsi tulivyo

Unyonge watusumbuwa sisi,

Na kuita mapendo yako.

kwa Roho tuliyeahidiwa,

Uzaifuni twabariki.

Wimbo 58 — kipande 4

Tukipiga hivi mwendo huu,

Twaelekea kwako, Ee Yesu,

Ndani yako hazina yetu,

Maji ya chem.chemu ya mbinguni

Na mkate wa wateule.

59.                  Wimbo 59

Wimbo 59 — kipande 1

Tangu asubui, mioyo yakubariki.

Mchana na usiku, tu mkononi mwako

kwa wana wako, wema wako haukomi

Tena watupenda bila hata kuchoka.

Wimbo 59 — kipande 2

Tunaomba kwako neema ya ajabu:

Utulishe leo na mkate wa mbingu;

Tunajingojea kwa musaada wako;

Daima watufunika na mkono wako.

Wimbo 59 — kipande 3

Roho wako Mungu atufundishe njia,

Kwa neno lako takatifu mioyoni!

Tukitiwa nguvu naye hakuna woga,

Na tupo washindi pamoja na Kristo.

Wimbo 59 — kipande 4

Tupo wasafiri, wageni duniani,

Moyo wetu unahaja ya mbinguni.

Ni mbinguni mwako, Mungu na baba wetu

Tutakapoingia kwa pendo lako.

Wimbo 59 — kipande 5

Utuchunge katika safari salama,

Hadi siku ya heri bila magumu,

Tutaonja pamoja uheri muzuri,

Wakati Yesu atakapo tupumuzisha.

60.                  Wimbo 60

Wimbo 60 — kipande 1

Sifaidiki wala kupoteza

Jangwani humu sina chaguo :

Hakuna pori hata jani bichi,

Hakuna maji yakuninywesha.

Wimbo 60 — kipande 2

Jangwani hakuna kimbilio,

Wala pumziko hata kidogo,

Kwa nini mimi nisimame bure

Ninapokaribia kufika?

Wimbo 60 — kipande 3

Jangwani mimi ninajua njia :

Njia ya pendo, neema na imani,

Nitakayoifwata bila shaka,

Kwani Mwokozi aliipasua.

Wimbo 60 — kipande 3

Njia ya nguvu ijaayo heri,

Ambamo yote ni salama tu ;

Iniongozayo toka duniani,

Ilinifike kwa Baba Mungu.

Wimbo 60 — kipande 4

Bila tamaa, bila kazi na woga,

Umenifundisha kukaa pale,

Nitaonja, pale patakatifu

Pumziko karibu nawedaima.

61.                  Wimbo 61

Wimbo 61 — kipande 1

Tuimbe, tuimbe katika wimbo safi

Pendo la Mwokozi

Neema yake amini

Siku zote ni mpya

Inaangaa sana

{Yeye mkubwa na muzuri

Tumsifu Bwana, (x2).}

Wimbo 61 — kipande 2

Tuimbe, tuimbe katika wimbo safi

Pendo la Mwokozi

Kiti cha neema

Fasi ya hakika

Kwa mioyo yetu

{Yeye mkubwa na muzuri} etc.

Wimbo 61 — kipande 3

Tuimbe, tuimbe katika wimbo safi

Pendo la Mwokozi

Yesu utukufuni

Ni ushindi wetu

Na heri yetu

{Yeye mkubwa na muzuri} etc.

62.                  Wimbo 62

Wimbo 62 — kipande 1

Sifa, uwezo na nguvu

Heshima kwake Mungu

Upendo na shukurani

Kwake Yesu Mwokozi.

Wimbo 62 — kipande 2

Mwokozi ulivikwa miiba

Damu yako’kamwangwa

Hata gazabu ya Mungu

Na Ikakulemea.

Wimbo 62 — kipande 3

Kwako ee Yesu mateso

Kilio, kifo, kuachwa

Na kwa sisi ukombozi

Wokovu, usamehe.

Wimbo 62 — kipande 4

Sifa, uwezo na nguvu

Heshima kwake Mungu

Upendo na shukurani

Kwake Yesu Mwokozi.